Chama cha walimu nchini (CWT), kimesema bado hakina maoni ya kutoa
kuhusiana na muswada wa sheria ya bodi ya walimu, ambao unatarajiwa
kuanza kujadiliwa na kamati ya Bunge ya huduma za jamii kabla ya
kupelekwa bungeni ili kuwa sheria.
.
Rais
wa CWT Leah Ulaya, ameieleza East Africa Breakfast ya East Africa Radio
kuwa kwa kushirikiana na wanasheria wao wataujadili kwa kina muswada
huo ambao unapendekeza kuanzishwa kwa bodi ya walimu itakayokuwa
ikisajili na kuwapa leseni walimu wote, na kutoruhusu mtu asiye na
leseni kufundisha.
“Tunaomba tupatiwe muda ndio tutoe maoni sahihi kwa kushirikiana na wanasheria wetu, kwa sasa hatuna majibu sahihi”,amesema Rais wa CWT.
Hayo yamejiri baada ya kuwasilishwa kwa muswada bungeni Mei 2 mwaka
huu na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako,
ambao ulipendekeza kuanzishwa bodi ya taaluma ya ualimu kama
utapitishwa na kuwa sheria, mwalimu hataruhusiwa kufundisha mpaka awe na
leseni.
Muswada huo ulisomwa kwa mara ya kwanza Juni mwaka huu ambapo Spika
wa Bunge, Job Ndugai, aliiagiza Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo
ya Jamii kuanza kuufanyia kazi ujadiliwe katika mkutano ujao.
“Tunaomba tupatiwe muda ndio tutoe maoni '' Rais wa CWT
Reviewed by jaqueline victorv
on
Tuesday, August 21, 2018
Rating: 5
No comments:
Post a Comment